WASHINGTON
Friday, 19 January 2018
Ripoti ya Shirika la kutetea haki za binaadamu la Human Right Watch ya mwaka 2018 imeangazia haki za binaadamu namna zilivyokiukwa katika mataifa kadhaa barani Afrika.
Ripoti
ya Shirika la
kutetea haki za binaadamu la
Human Right Watch ya mwaka 2018 imeangazia haki za binaadamu namna
zilivyokiukwa katika mataifa kadhaa barani Afrika.
Ikianza na Tanzania, ripoti hiyo inasema baada
ya kuingia serikali
awamu ya tano ilidhamiria kuondoa tatizo la rushwa serikalini na
kuongeza uwajibikaji kwa manufaa ya wananchi wa kawaida, lakini badala yake
uhuru wa kukosoa umekandamizwa ikiwemo kufungwa kwa vyombo
vya habari.
Aidha imeeleza kuwa watetezi wa haki za binadamu, wanaharakati wa asasi
za kiraia na maafisa waandamizi wa Umoja wa Mataifa wamekumbana na aina
mbalimbali za vitisho na kuwekwa vizuizini bila sababu za msingi kunakofanywa
na mamlaka za serikali.
Nchini Kenya nako Shirika hilo limebaini kuwa mauaji yaliyofanywa na polisi katika mitaa
ya mabanda hayakuchunguzwa hadi leo.
Aidha
katika kipindi cha kabla na baada ya uchaguzi shirika hilo limesema polisi na
vikosi vingine vya usalama vimetumia nguvu kupita kiasi kuwakabili
waandamanaji hasa katika ngome za upinzani.
Chanzo: Dw swahili
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Featured post
MASIKINI WEEE!!!!! KICHANGA CHA SIKU MOJA CHAOKOTWA KATIKA KIWANJA CHA MPIRA AZIMIO
Na;Ezelina Yuda Mtoto mchanga mwenye jinsia ya Kike anayekadiriwa kuwa wa siku 1 ameokotwa akiwa hai kandokando ya uwanja wa azimio ...
-
Kabale, Uganda. Mpinzani mkuu wa Uganda na kiongozi wa Forum for Democratic Change (FDC) Dk Kizza Besigye amekamatwa. ...
-
KATAVI Shule ya msingi Misunkumilo iliyopo Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa na madawati...
-
KIGOMA . VITUO vya afya Uvinza na Nguruka vilivyopo wilayani Uvinza Mkoa wa Kigoma vinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo yaup...

No comments:
Post a Comment