Thursday, 7 December 2017
Mauaji Kibiti, chanzo cha Mwandishi kupotea?
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) wanaamini
kutoweka kwa mwandishi Azory Gwanda wa gazeti la Mwananchi kwa siku 17 sasa ni
kwa nia mbaya.
Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri Teofile Makunga
anasema kama mwandishi huyu angekuwa anashikiliwa na vyombo vya usalama kwa
sababu yoyote angetakiwa kuwa amefikishwa mahakamani kufikia sasa.
Mkurugenzi wa gazeti la Mwananchi Francis Nanai
ameomba vyombo vya ulinzi na usalama kuzidisha kasi ya kumtafuta mwanahabari
huyo ambaye ametoweka kwa zaidi ya siku kumi sasa.
Wahariri wanapanga kufanya maandamano ya kushinikiza
kuzidishwa kazi kwa msako huo yatakayoanzia mnazi mmoja hadi makao makuu ya
wizara ya mambo ya ndani jijini Dar es Salaam.
Bwana Gwanda ni mmoja wa waaandishi wa kwanza
kabisa kuripoti kwa kina juu ya mfululizo wa mauwaji yaliyokuwa yakitekelezwa
na watu wasiojulikana yaliyowalenga polisi na viongozi wa mji huo.
Source Eatv
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Featured post
MASIKINI WEEE!!!!! KICHANGA CHA SIKU MOJA CHAOKOTWA KATIKA KIWANJA CHA MPIRA AZIMIO
Na;Ezelina Yuda Mtoto mchanga mwenye jinsia ya Kike anayekadiriwa kuwa wa siku 1 ameokotwa akiwa hai kandokando ya uwanja wa azimio ...
-
Kabale, Uganda. Mpinzani mkuu wa Uganda na kiongozi wa Forum for Democratic Change (FDC) Dk Kizza Besigye amekamatwa. ...
-
Serikali ya mtaa wa Kampuni Kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imewaomba wataalamu wa maji Manispaa ya Mpanda kuchungu...
-
TABORA Wananchi wa kijiji cha makibo kata ya Nyahua wilayani sikonge mkoani Tabora wamelalamikia ujenzi wa madaraja mabovu ya baraba...
No comments:
Post a Comment