Tuesday, 11 July 2017
Mbunge wa jimbo la Nsimbo mkoani Katavi Mh: Richard Mbogo ametoa wito kwa serikali kuongeza muda kabla ya kutekeleza bomoa bomoa kwa makazi yalio katika hifadhi ya reli katika Kata ya Ugala.
Amesema hayo mapema jana alipokuwa akizungumza na Mpanda radio fm ambapo amefafanua kuwa endapo zoezi hilo litatekelezwa kwa muda ulio wekwa litaiathiri jamii kwa kiwango kikubwa kutokana na kutokuwepo kwa makazi mbadala.
Katika hatua nyingine amezitaja baadhi ya hatua anazo zichukua kuwa ni pamoja na kufanya mazungumzo na msemaji wa shirika la reli kwa mkoa wa Katavi na Tabora ili kupata ufumbuzi ambao hauta waumiza wananchi wa eneo hilo.
Nitakribani siku kumi na moja tangu shirika la reli kuwataka wananchi wote walio jenga nyumba katika hifadhi ya reli kuzibomoa wao wenyewe kwa muda wa mwezi mmoja.
Ila itakapo fika muda walio uweka kuisha bila kuzibomoa shirika litaziboa pia litawatoza fidia ya kuzibomolea nyumba hizo zoezi la kubomoa nyumba ambazo zipo katika hifadhi ya reli.
Linategemewa kuanza tangu sasa kwa wale wote waliowekewa alama ya X pia kufikia tare 29 reli nao wataanza kubomoa kwa fain kwa wale wote ambao watakuwa wamekaidi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Featured post
MASIKINI WEEE!!!!! KICHANGA CHA SIKU MOJA CHAOKOTWA KATIKA KIWANJA CHA MPIRA AZIMIO
Na;Ezelina Yuda Mtoto mchanga mwenye jinsia ya Kike anayekadiriwa kuwa wa siku 1 ameokotwa akiwa hai kandokando ya uwanja wa azimio ...
-
KATAVI Shule ya msingi Misunkumilo iliyopo Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa na madawati...
-
KIGOMA . VITUO vya afya Uvinza na Nguruka vilivyopo wilayani Uvinza Mkoa wa Kigoma vinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo yaup...
-
NSIMBO Soko la Katumba Mnyaki linalomilikiwa na halamshauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi halina choo tangu kuanzishwa kwake hali...

No comments:
Post a Comment