MPANDA.
Mwenyekiti wa Chama cha madreva
pikipiki za tairi tatu maarufu bajaji halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani
Katavi Bw.Rashid Rashid ametangaza kujiuzuru nafasi hiyo.
Katika taarifa yake ambayo ameitoa
leo Bw.Rashid amesema, miongoni mwa sababu za kujiuzulu kwake ni pamoja na
kukosa ushirikiano kutoka kwa madereva wenzake,ukosefu wa ushirikiano kwa kamati
yake na kutotekelezwa kwa mipango mbalimbali wanayoipanga kama chama.
Aidha amesema changamoto iliyopo kwa
sasa ni mgawanyiko wa wamiliki bajaji upande wa watumishi wa serikali kutozingatia
kanuni na taratibu za umiliki wa chombo hicho cha usafiri pamoja na watu
binafsi kulipishwa faini mara kwa mara bila utaratibu.
Mapema mwaka huu,baadhi ya madereva
bajaji walikuwa wakilalamika kutozwa fedha mpaka elfu arobaini ili chombo chake
cha usafiri kipewe namba ya usajili kwa ajili ya kuendesha shughuli zao wakiwa
katika maegesho wanayopangiwa.
Chanzo: Issack Gerald


No comments:
Post a Comment