Tuesday, 9 January 2018
Msemaji wa Umoja wa Mataifa Bw Stephane Dujarric amesema takriban watu 700 wamepoteza makazi yao kutokana na operesheni za kijeshi dhidi ya waasi wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Kundi la IS zilizofanyika mjini Kirkuk, Iraq tangu Alhamisi iliyopita.
BAGHDAD
Msemaji wa Umoja wa Mataifa Bw Stephane Dujarric
amesema takriban watu 700 wamepoteza makazi yao kutokana na operesheni za
kijeshi dhidi ya waasi wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Kundi la IS
zilizofanyika mjini Kirkuk, Iraq tangu Alhamisi iliyopita.
Msemaji huyo amesema Ofisi ya uratibu wa misaada
ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa OCHA imeripoti kuwa watu hao waliokimbia
mapambano kwenye eneo la Hawija wanahamishiwa kambi ya wakimbizi iliyoko karibu
na Daquq, ambako watapewa msaada wa kibinadamu.
Msemaji huyo pia ameongeza kuwa utoaji wa
misaada ya kibinadamu katika eneo la Hawija umesimamishwa kutokana na sababu za
usalama, na utarejeshwa mara baada ya operesheni ya kijeshi kukamilika.
Chanzo: Dw swahili
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Featured post
MASIKINI WEEE!!!!! KICHANGA CHA SIKU MOJA CHAOKOTWA KATIKA KIWANJA CHA MPIRA AZIMIO
Na;Ezelina Yuda Mtoto mchanga mwenye jinsia ya Kike anayekadiriwa kuwa wa siku 1 ameokotwa akiwa hai kandokando ya uwanja wa azimio ...
-
Kabale, Uganda. Mpinzani mkuu wa Uganda na kiongozi wa Forum for Democratic Change (FDC) Dk Kizza Besigye amekamatwa. ...
-
KIGOMA . VITUO vya afya Uvinza na Nguruka vilivyopo wilayani Uvinza Mkoa wa Kigoma vinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo yaup...
-
NSIMBO Soko la Katumba Mnyaki linalomilikiwa na halamshauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi halina choo tangu kuanzishwa kwake hali...

No comments:
Post a Comment