MOSHI
Friday, 16 February 2018
Mahakama Kuu imemhukumu kifungo cha maisha jela raia wa Lithuania, Christina Biskavskaja baada ya kupatikana na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya kwenda Ubelgiji
Mahakama
Kuu imemhukumu kifungo cha maisha jela raia wa Lithuania, Christina Biskavskaja
baada ya kupatikana na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya kwenda Ubelgiji.
Christina
ambaye ni mwanamuziki katika Jiji la Kaunas, amekamatwa Agosti 28, 2012 saa tisa
alasiri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) akisafirisha
gramu 3,775.26 za heroine zenye thamani ya Sh169 milioni.
Hukumu hiyo
imetolelwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, Aishiel Sumari amesema ushahidi wa mashahidi saba wa upande wa mashtaka ni mzito na
umethibitisha shtaka dhidi ya mshtakiwa huyo.
Jaji Sumari
aliukataa utetezi wa mshtakiwa kuwa alibambikiwa kesi hiyo na polisi wa
Tanzania na kuhoji hilo linawezekanaje wakati mashahidi wa upande wa mashtaka
walikuwa hawafahamiani na mshtakiwa.
Chanzo: Mwananchi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Featured post
MASIKINI WEEE!!!!! KICHANGA CHA SIKU MOJA CHAOKOTWA KATIKA KIWANJA CHA MPIRA AZIMIO
Na;Ezelina Yuda Mtoto mchanga mwenye jinsia ya Kike anayekadiriwa kuwa wa siku 1 ameokotwa akiwa hai kandokando ya uwanja wa azimio ...
-
Kabale, Uganda. Mpinzani mkuu wa Uganda na kiongozi wa Forum for Democratic Change (FDC) Dk Kizza Besigye amekamatwa. ...
-
Serikali ya mtaa wa Kampuni Kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imewaomba wataalamu wa maji Manispaa ya Mpanda kuchungu...
-
TABORA Wananchi wa kijiji cha makibo kata ya Nyahua wilayani sikonge mkoani Tabora wamelalamikia ujenzi wa madaraja mabovu ya baraba...

No comments:
Post a Comment