Wednesday, 21 February 2018
Mkazi wa kata ya Inyonga Halmashauri ya Wilaya ya Mlele anayefahamika kwa jina la Amani Silveri Pendelesi amefikishwa mahakamani kwa kosa la kuingia nchini bila kuwa na vibali maalumu.
MLELE
Mkazi
wa kata ya Inyonga Halmashauri ya Wilaya ya Mlele anayefahamika kwa jina la
Amani Silveri Pendelesi amefikishwa mahakamani kwa kosa la kuingia nchini bila
kuwa na vibali maalumu.
Tukio
hilo limetokea tarehe 14 mwezi huu katika kata ya inyonga mtuhumiwa mwenye umri wa miaka 35 raia wa
Burundi amekamatwa wakati akijaribu
kujipatia kitambulisho cha uraia wa Tanzania ambacho ni kinyume cha sheria za
nchi hii..
Kesi
hiyo imesikilizwa leo katika Mahakam ya hakimu mkazi mkoani katavi mbele ya
hakimu Omari Hassani Kingwele na mwendesha mashtaka wa uhamiaji Joseph Bajagae
na mshitakiwa kukiri kutenda kosa hilo.
Hata
hivyo mshitakiwa huyo amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela au kutoa faini
ya shilingi laki tano za kitanzania.
Kuingia nchini bila kibali ni kinyume na kifungu cha
45 sehemu ya kwanza cha sheria ya uhamiaji na ukurasa wa saba sura ya 54 kama
ilivyofanyiwa mabadiliko mwaka 2016 imehukumu kesi hiyo.
Chanzo:Furaha Kimondo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Featured post
MASIKINI WEEE!!!!! KICHANGA CHA SIKU MOJA CHAOKOTWA KATIKA KIWANJA CHA MPIRA AZIMIO
Na;Ezelina Yuda Mtoto mchanga mwenye jinsia ya Kike anayekadiriwa kuwa wa siku 1 ameokotwa akiwa hai kandokando ya uwanja wa azimio ...
-
Kabale, Uganda. Mpinzani mkuu wa Uganda na kiongozi wa Forum for Democratic Change (FDC) Dk Kizza Besigye amekamatwa. ...
-
KATAVI Shule ya msingi Misunkumilo iliyopo Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa na madawati...
-
KIGOMA . VITUO vya afya Uvinza na Nguruka vilivyopo wilayani Uvinza Mkoa wa Kigoma vinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo yaup...

No comments:
Post a Comment